Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2018

USISUMBUE AKILI YAKO NA MANENO YA KUAMBIWA KITU FULANI KINALIPA!

​ USISUMBUE AKILI YAKO NA MANENO YA KUAMBIWA KITU FLANI KINALIPA:- ​ ​ MFANO:- ​ Ukipata nafasi ya kufika kule ​ Mbozi, Mbeya ​ ukakutana na habari za watu wanaotajirika kutokana na ​ kilimo cha kahawa ​, kwa kweli unaweza kuwehuka, na kujiona kama mtu uliyechelewa kweli kweli. Wakati unarudi, kama ukishuka ​ Mafinga, Njombe ​ na kufuatilia stori na kutazama mamilionea walioupata umilionea kutokana na ​ biashara ya miti na mbao ​, unaweza kudhani kwamba hapa duniani fursa inayowatoa watu kiuharaka ni mbao pekee! Pitia maeneo ya ​ Ruaha Mbuyuni, Iringa ​ kutana na wakulima wa ​ nyanya na vitunguu ​ wakikuonesha coaster walizonunua kwa kilimo cha msimu mmoja pekee. Aisee kama una akiba utanunua shamba muda huo huo na kuachana na ajira kama ulikuwa mwajiriwa. Ukitoka pale ukaenda mpaka ​ Mang'ula na Ifakara Morogoro, ​ ukakutana na habari za watu wanavyopiga hela kwenye ​ mpunga ​, kichwa chako kinaweza kuwaka moto. Unaweza kujizaba vibao na kujimaindi, afu utajiuliza, ...